Saturday 19 January 2008

mashairi ya kido

kuanzia sasa jiandae kupata mashairi mapya, kila mungu ataponijaalia kuklaa katika ngamiza na kuandika nilichojaaliwa kwa siku hiyo. kwa leo anza na hili shairi dogo...



GOD OF MANY COLOUR



my father use to tll me

God is one

Wasn't born

and all alone



But now aday's

People lost

They almost

like ghost



Every group have God

who named

Always instead

By race and colour



Who is the real one

I want to follow

Before him to bow

ooh!!.. my mind allow



The God of many colour

I'm with you

White, Black or Blue

They praise your name







LOVE IS.....



Love is every where

it exist

For one who care

can't resist

And those who aware

fail at last



I always pray to God

to get one

Who will raise my mood

being fine

ooh!! yes i understand

love is line



Many people tend to cry

for love

make their soul fly

to deserve

but most of them lay

to achieve



I lost my cute GRACE

for jelous

I have no one to replace

it's dangerous

Her eyes was like spice

ooh!! hopelesness



Now im all alone

I cry!

Everything i concern

now it fly

The tears it drown

cant dry!







PESA SUMU



pesa sumu ya furaha, ila huleta mapenzi

waliokosa shabaha, huniona mpuuzi

ajabu nao huhaha, kuwaridhisha vipenzi

dunia yetu ya sasa, bila pesa hupendeki



ajabu ya jambo hili, halipati magunduzi

wengi tunastahamili, na nyoyo kupata ganzi

hudhani tunastahili, kwa udhati wa mapenzi

kupenda hakutoshi kitu, watu wanataka pesa!



pendo hapewi baghili, nimefanya uchunguzi

wake wana maufili, na waume ni washenzi

mapenzi yenye adili, kuyapata hatuwezi

mmoja akiwa mwema, wa pili huharibika



mapenzi janga la kiu, na hilo ni toka enzi

mtoa ana dharau, hafikirii ijazi

mpokea ni bahau, mchafu mwenye kutuzi

al-khitaju hanitha, lau kanna rijaalu..



wakatabahu bakungwi, ni mwisho wa maongezi

ajifaae hanangwi, hupata mambo azizi

mapendo ni kama mwangwi, kuuzuia huwezi

na kazi ipo kwa yule, mpenda asiependwa





PUMZI



pumzi zina hadaa, na kutupa kiburi

tena bila ridhaa, ya mola maamuri

nyoyo zimetufubaa, hatuogopi kaburi



maudhi na shufaa, hupeleka umuri

mengi yasiyofaa, hupulizwa uturi

unyonge na zanaa, waja hayawaghuri



dunia kama jaa, kawaida si zuri

taka zisizofaa, ndiwo huu umuri

maisha ni kichaa, waja hatufikiri



wevi wa makataa, husubiri kujiri

hawangoji ridhaa, kukutia kabari

wangeiba asaa, hutukata umuri!!!..

No comments: