1.moyo umefunga penzi, la mahabubu fulani
keshapo ninalienzi, lisidondoke changani
wanijiliapo wezi, huwa mfarakanoni
ajabu moja ni kuwa, simjui mja huyo
2.hapata wivu wa nafsi, nikaungua rohoni
nikabanguliwa rasi, ugonjwa nisibaini
tabu zisizo kiasi, kuninahili moyoni
ajabu moja ni kuwa, simjui mja huyo
3.mapenzi haya ya ghibu, kuwa kwake siamini
yalianza taratibu, kuingia akilini
sasa ndo nahisi tabu, mapenzi kunitahini
ajabu moja ni kuwa, simjui mja huyo
4.awali lihisi tamu, na furahiko ndotoni
hatekenya milizamu, nilalapo kitandani
kumbe najinywesha sumu, ya teseko maishani
ajabu moja ni kuwa, simjui mja huyo
5.akija huchekacheka, na kudekewa mwilini
pwani tukarukaruka, mfano mahayawani
sabahi kikurupuka, pekee hajibaini
ajabu moja ni kuwa, simjui mja huyo
6.ana uso wa duara, huburudisha aini
na kifua cha kufura, mwenyezi hakumhini
miguu ilo imara, hufurahisha machoni
ajabu moja ni kuwa, simjui mja huyo
7.ana macho ya kung'ara, mithali yake sioni
kope zake zimechora, mfano wa asumini
na libasi za sitara, kama zatoka peponi
ajabu moja ni kuwa, simjui mja huyo
8.nimekwenda kwa waganga, zindiko kulibaini
mitishamba kunisinga, kama mwari mafundoni
hirizi wakanifunga, kuenea maungoni
ajabu moja ni kuwa, simjui mja huyo
9.kila jambo halikuwa, ndugu nisaidieni
vitabu nimebukuwa, vya uchawi na vya dini
nimebaki naungua, mola hanipi idhini
ajabu moja ni kuwa, simjui mja huyo
10.wakatabahu shairi, wajuvi nielezeni
kwa wale wanofasiri, ruwiya za mapenzini
naomba yenu nadhari, asaa nimbaini
ajabu moja ni kuwa, simjui mja huyo
Thursday 24 January 2008
Wednesday 23 January 2008
LADHA YA USHAIRI
AKILI KUZIHARIBU
1.wapungufu wa akili, kisha tunaziharibu
kwa maji yalo dhalili, twaadhirika ajabu
wasomi wenye adili, vileo huwatulubu
pombe hutudhalulusha, na kurufaisha akili
2.kwa zetu mbaya fiili, mola anatuadhibu
makatazo hatujali, tu wima kama bawabu
mwisho wa siku twafeli, peponi twajitanibu
pombe hutudhalilisha, na kurufaisha akili
3.twazitia uasili, amali ziso adabu
vinywaji vyenye mushkeli, twaviita vya mababu
mawazo ya kibaghili, viumbe yametusibu
pombe hutudhalilisha, na kurufaisha akili
4.wa moja hashiki mbili, ya busara na ulabu
ubongo hatuujali, hulegeza sukurubu
nyoyo hupata ajali, tukawa kama mabubu
pombe hutudhalilisha, na kurufaisha akili
5.himila wanohimili, bure hujitia tabu
hufura yao miili, na nyuso kufanya gubu
mtoto akiwasili, wakunga huwatulubu
pombe hutudhalilisha, na kurufaisha akili
6.nawaasa kula hali, mtenzi nawaadibu
kwa uchache wa kauli, penye makosa natubu
natetea maadili, siandiki kwa ghadhabu
pombe hutudhalilisha, na kurufaisha akili
MAISHA
1.maisha yanatutesa, na kutunyima huruma
hupatwa na vingi visa, kwa chukizo na hujuma
wengi hupata garasa, hata wanapojituma
2.maisha yana mikasa, kila siku kila juma
dunia hutikisika, kwa dhambi zenye kuuma
kama tulo na darasa, matusi tunavyosema
3.maisha yana makosa, mwanadamu hana jema
kama tulo na ruhusa, kwa vitendo vya uchama
tena hayo yote tisa, kumi kumtusi mama?
4.maisha yana usasa, cha zamani siyo chema
mcha mungu hukutesa, kwa kuwarudisha nyuma
ukihudhuria kesa, na fedha hukuazima
5.maisha yana anasa, akili usipotuma
vitamu hutovikosa, madhambi ukiyachuma
mwisho wale vibubusa, hulia na kuchutama
UTUMWA WA MAOVU
1.utumwaji wa maovu, hudhihaki milizamu
hukomaa kama kovu, ridhio lake ni hamu
moyo hupata machovu, na kulia madhulumu
ila mtumwa wa dhambi, hutubia akaacha
2.ovu halina utuvu, hufanya mwenye nidhamu
keshapo hushika shavu, kulia kibahaimu
akidai maonevu, yeye yamemstakimu
ila ajabu ya mungu, kesho hurudia tena!
3.hana ustahamilivu, muovu akikasimu
humnasa kama wavu, ubaya kwa wanadamu
tena huwa ni shupavu, hata jambole litimu
hapo hupata wasaa, akamkumbuka mungu
4.watovu wa usikivu, wovu washikwapo hamu
hupatwa na maumivu, katika zao fahamu
hawawi ni wakatavu, hudhani ni isilamu
hawaombeleki dua, nyoyo zimepigwa chapa
5.na hivi vina vya VU, vinaninyima kalamu
mfano wake VVU, umuri kunidhulumu
hapa nafanya kitovu, nimezidiwa elimu
vina vimeniishia, shairi laendelea.
1.wapungufu wa akili, kisha tunaziharibu
kwa maji yalo dhalili, twaadhirika ajabu
wasomi wenye adili, vileo huwatulubu
pombe hutudhalulusha, na kurufaisha akili
2.kwa zetu mbaya fiili, mola anatuadhibu
makatazo hatujali, tu wima kama bawabu
mwisho wa siku twafeli, peponi twajitanibu
pombe hutudhalilisha, na kurufaisha akili
3.twazitia uasili, amali ziso adabu
vinywaji vyenye mushkeli, twaviita vya mababu
mawazo ya kibaghili, viumbe yametusibu
pombe hutudhalilisha, na kurufaisha akili
4.wa moja hashiki mbili, ya busara na ulabu
ubongo hatuujali, hulegeza sukurubu
nyoyo hupata ajali, tukawa kama mabubu
pombe hutudhalilisha, na kurufaisha akili
5.himila wanohimili, bure hujitia tabu
hufura yao miili, na nyuso kufanya gubu
mtoto akiwasili, wakunga huwatulubu
pombe hutudhalilisha, na kurufaisha akili
6.nawaasa kula hali, mtenzi nawaadibu
kwa uchache wa kauli, penye makosa natubu
natetea maadili, siandiki kwa ghadhabu
pombe hutudhalilisha, na kurufaisha akili
MAISHA
1.maisha yanatutesa, na kutunyima huruma
hupatwa na vingi visa, kwa chukizo na hujuma
wengi hupata garasa, hata wanapojituma
2.maisha yana mikasa, kila siku kila juma
dunia hutikisika, kwa dhambi zenye kuuma
kama tulo na darasa, matusi tunavyosema
3.maisha yana makosa, mwanadamu hana jema
kama tulo na ruhusa, kwa vitendo vya uchama
tena hayo yote tisa, kumi kumtusi mama?
4.maisha yana usasa, cha zamani siyo chema
mcha mungu hukutesa, kwa kuwarudisha nyuma
ukihudhuria kesa, na fedha hukuazima
5.maisha yana anasa, akili usipotuma
vitamu hutovikosa, madhambi ukiyachuma
mwisho wale vibubusa, hulia na kuchutama
UTUMWA WA MAOVU
1.utumwaji wa maovu, hudhihaki milizamu
hukomaa kama kovu, ridhio lake ni hamu
moyo hupata machovu, na kulia madhulumu
ila mtumwa wa dhambi, hutubia akaacha
2.ovu halina utuvu, hufanya mwenye nidhamu
keshapo hushika shavu, kulia kibahaimu
akidai maonevu, yeye yamemstakimu
ila ajabu ya mungu, kesho hurudia tena!
3.hana ustahamilivu, muovu akikasimu
humnasa kama wavu, ubaya kwa wanadamu
tena huwa ni shupavu, hata jambole litimu
hapo hupata wasaa, akamkumbuka mungu
4.watovu wa usikivu, wovu washikwapo hamu
hupatwa na maumivu, katika zao fahamu
hawawi ni wakatavu, hudhani ni isilamu
hawaombeleki dua, nyoyo zimepigwa chapa
5.na hivi vina vya VU, vinaninyima kalamu
mfano wake VVU, umuri kunidhulumu
hapa nafanya kitovu, nimezidiwa elimu
vina vimeniishia, shairi laendelea.
Sunday 20 January 2008
taaluma ya uandishi wa habari
taaluma ya uandishi, imejitokeza
ni kazi ya aushi, yapendeza
wachukiao ni wabishi, tutawabeza
karibuni tanzania, uandishi unangaa
ni kazi ya aushi, yapendeza
wachukiao ni wabishi, tutawabeza
karibuni tanzania, uandishi unangaa
urembo
urembo tanzania, unapendeza
kwa wote wenye nia, vema kujitokeza
kwa kheri na taania, tutawapongeza
kwa wote wenye nia, vema kujitokeza
kwa kheri na taania, tutawapongeza
Saturday 19 January 2008
mashairi ya kido
kuanzia sasa jiandae kupata mashairi mapya, kila mungu ataponijaalia kuklaa katika ngamiza na kuandika nilichojaaliwa kwa siku hiyo. kwa leo anza na hili shairi dogo...
GOD OF MANY COLOUR
my father use to tll me
God is one
Wasn't born
and all alone
But now aday's
People lost
They almost
like ghost
Every group have God
who named
Always instead
By race and colour
Who is the real one
I want to follow
Before him to bow
ooh!!.. my mind allow
The God of many colour
I'm with you
White, Black or Blue
They praise your name
LOVE IS.....
Love is every where
it exist
For one who care
can't resist
And those who aware
fail at last
I always pray to God
to get one
Who will raise my mood
being fine
ooh!! yes i understand
love is line
Many people tend to cry
for love
make their soul fly
to deserve
but most of them lay
to achieve
I lost my cute GRACE
for jelous
I have no one to replace
it's dangerous
Her eyes was like spice
ooh!! hopelesness
Now im all alone
I cry!
Everything i concern
now it fly
The tears it drown
cant dry!
PESA SUMU
pesa sumu ya furaha, ila huleta mapenzi
waliokosa shabaha, huniona mpuuzi
ajabu nao huhaha, kuwaridhisha vipenzi
dunia yetu ya sasa, bila pesa hupendeki
ajabu ya jambo hili, halipati magunduzi
wengi tunastahamili, na nyoyo kupata ganzi
hudhani tunastahili, kwa udhati wa mapenzi
kupenda hakutoshi kitu, watu wanataka pesa!
pendo hapewi baghili, nimefanya uchunguzi
wake wana maufili, na waume ni washenzi
mapenzi yenye adili, kuyapata hatuwezi
mmoja akiwa mwema, wa pili huharibika
mapenzi janga la kiu, na hilo ni toka enzi
mtoa ana dharau, hafikirii ijazi
mpokea ni bahau, mchafu mwenye kutuzi
al-khitaju hanitha, lau kanna rijaalu..
wakatabahu bakungwi, ni mwisho wa maongezi
ajifaae hanangwi, hupata mambo azizi
mapendo ni kama mwangwi, kuuzuia huwezi
na kazi ipo kwa yule, mpenda asiependwa
PUMZI
pumzi zina hadaa, na kutupa kiburi
tena bila ridhaa, ya mola maamuri
nyoyo zimetufubaa, hatuogopi kaburi
maudhi na shufaa, hupeleka umuri
mengi yasiyofaa, hupulizwa uturi
unyonge na zanaa, waja hayawaghuri
dunia kama jaa, kawaida si zuri
taka zisizofaa, ndiwo huu umuri
maisha ni kichaa, waja hatufikiri
wevi wa makataa, husubiri kujiri
hawangoji ridhaa, kukutia kabari
wangeiba asaa, hutukata umuri!!!..
GOD OF MANY COLOUR
my father use to tll me
God is one
Wasn't born
and all alone
But now aday's
People lost
They almost
like ghost
Every group have God
who named
Always instead
By race and colour
Who is the real one
I want to follow
Before him to bow
ooh!!.. my mind allow
The God of many colour
I'm with you
White, Black or Blue
They praise your name
LOVE IS.....
Love is every where
it exist
For one who care
can't resist
And those who aware
fail at last
I always pray to God
to get one
Who will raise my mood
being fine
ooh!! yes i understand
love is line
Many people tend to cry
for love
make their soul fly
to deserve
but most of them lay
to achieve
I lost my cute GRACE
for jelous
I have no one to replace
it's dangerous
Her eyes was like spice
ooh!! hopelesness
Now im all alone
I cry!
Everything i concern
now it fly
The tears it drown
cant dry!
PESA SUMU
pesa sumu ya furaha, ila huleta mapenzi
waliokosa shabaha, huniona mpuuzi
ajabu nao huhaha, kuwaridhisha vipenzi
dunia yetu ya sasa, bila pesa hupendeki
ajabu ya jambo hili, halipati magunduzi
wengi tunastahamili, na nyoyo kupata ganzi
hudhani tunastahili, kwa udhati wa mapenzi
kupenda hakutoshi kitu, watu wanataka pesa!
pendo hapewi baghili, nimefanya uchunguzi
wake wana maufili, na waume ni washenzi
mapenzi yenye adili, kuyapata hatuwezi
mmoja akiwa mwema, wa pili huharibika
mapenzi janga la kiu, na hilo ni toka enzi
mtoa ana dharau, hafikirii ijazi
mpokea ni bahau, mchafu mwenye kutuzi
al-khitaju hanitha, lau kanna rijaalu..
wakatabahu bakungwi, ni mwisho wa maongezi
ajifaae hanangwi, hupata mambo azizi
mapendo ni kama mwangwi, kuuzuia huwezi
na kazi ipo kwa yule, mpenda asiependwa
PUMZI
pumzi zina hadaa, na kutupa kiburi
tena bila ridhaa, ya mola maamuri
nyoyo zimetufubaa, hatuogopi kaburi
maudhi na shufaa, hupeleka umuri
mengi yasiyofaa, hupulizwa uturi
unyonge na zanaa, waja hayawaghuri
dunia kama jaa, kawaida si zuri
taka zisizofaa, ndiwo huu umuri
maisha ni kichaa, waja hatufikiri
wevi wa makataa, husubiri kujiri
hawangoji ridhaa, kukutia kabari
wangeiba asaa, hutukata umuri!!!..
Friday 18 January 2008
ushairi Tanzania
naanza kwa maamkizi ya kitanzania, wakubwa shikamooni na wadogo wa makamo yangu habari za leo.
ushairi ulianza karne nyingi zilizopita, lakini fasihi kwa ujumla ilianza tangu kutambulika kwa lugha. nami naamini kuanza kuwepo wakaazi ndani ya tanzania ambapo awali ikitambulika kama Tanganyika na sitambui kabla ya Tanganyika ilikuwa ikitambuliwa kwa jina gani, maana twaambia na historia kuwa jina hili Tanganyika lililwetwa na wakoloni.
kazi za kijamii ndizo zilizoivumbua sanaa ya ushairi hasa, kadhalika mambo ya kiutawala na unyonyaji ndivyo vilivyokuja kuiendeleza na kuitilia vidoko sanaa hii. ingwa wapo watu waso fikira wala uzalendo wanaodiriki kusema kuwa sanaa ya ushairi ililetwa na waarabu. mawe!.. kamwe sikubaliani na ukweli huu.
ushairi ni wa kale, anaebishana aje
tangu wana na wavyele, lugha yetu waitaje
sikizeni kwa makele, tabia msinifuje
mkadai ni mtovu, historia kuipinda
hicho ni kitambulisho changu tu katika blogu hii, nina muda mchache sana wa kukaa na ngamiza, wakoloni wanaiita 'computer'. hivyo kunifanya kuwa na kauli ndogo na ulimi mfupi usokidhi matakwa ya wasikizaji na wasomaji wangu, poleni kwa hilo.
lakini mungu akinipa uhai na afia njema nitauendeleza mjadala huu kwa mifano hai na marejeo mema ya waandishi walowahi kuingia katika mjadala huu mzito mpaka mungu akazirufaisha roho zao kwa kuzipeleka kusikorudi.
saadan S kandoro, alitaabika sana
kwa tungo na mishororo, pambo za beti na vina
kuwarudisha watoro, lugha waloitukana
na mapurofesa lukuki, wa BAKITA na TUKI
HAFIDH A.KIDO (TOTO LA BAKUNGWI)
SIMU 0713593894.
BOX 1256
TANGA -TANZANIA
19-10-2008(AD)
10-MFUNGO NNE-1429(AH)
ushairi ulianza karne nyingi zilizopita, lakini fasihi kwa ujumla ilianza tangu kutambulika kwa lugha. nami naamini kuanza kuwepo wakaazi ndani ya tanzania ambapo awali ikitambulika kama Tanganyika na sitambui kabla ya Tanganyika ilikuwa ikitambuliwa kwa jina gani, maana twaambia na historia kuwa jina hili Tanganyika lililwetwa na wakoloni.
kazi za kijamii ndizo zilizoivumbua sanaa ya ushairi hasa, kadhalika mambo ya kiutawala na unyonyaji ndivyo vilivyokuja kuiendeleza na kuitilia vidoko sanaa hii. ingwa wapo watu waso fikira wala uzalendo wanaodiriki kusema kuwa sanaa ya ushairi ililetwa na waarabu. mawe!.. kamwe sikubaliani na ukweli huu.
ushairi ni wa kale, anaebishana aje
tangu wana na wavyele, lugha yetu waitaje
sikizeni kwa makele, tabia msinifuje
mkadai ni mtovu, historia kuipinda
hicho ni kitambulisho changu tu katika blogu hii, nina muda mchache sana wa kukaa na ngamiza, wakoloni wanaiita 'computer'. hivyo kunifanya kuwa na kauli ndogo na ulimi mfupi usokidhi matakwa ya wasikizaji na wasomaji wangu, poleni kwa hilo.
lakini mungu akinipa uhai na afia njema nitauendeleza mjadala huu kwa mifano hai na marejeo mema ya waandishi walowahi kuingia katika mjadala huu mzito mpaka mungu akazirufaisha roho zao kwa kuzipeleka kusikorudi.
saadan S kandoro, alitaabika sana
kwa tungo na mishororo, pambo za beti na vina
kuwarudisha watoro, lugha waloitukana
na mapurofesa lukuki, wa BAKITA na TUKI
HAFIDH A.KIDO (TOTO LA BAKUNGWI)
SIMU 0713593894.
BOX 1256
TANGA -TANZANIA
19-10-2008(AD)
10-MFUNGO NNE-1429(AH)
Subscribe to:
Posts (Atom)